Jinsi ya kuandika KITABU kikubwa kwa namna ya kawaida


Mwaka juzi nilitoa Kitabu CHANGU cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO. Kwenye Kitabu HIKI nimeeleza hatua kwa hatua jinsi ambavyo unaweza kufikia malengo na ndoto kubwa kwenye maisha.

Mmoja wa wasomaji wa Kitabu hicho alinipigia simu baada ya kuwa anlmekisona na kuniambia kuwa ana ndoto ya kuandika tamthiliya. Niliongeaa Naye na kumtakia kila la kheri.

Sasa juzi nilimpigia mwenyewe. Tukaanza kuongea na nikamwuliza mwenendo wa kitabu chake.

Ndipo aliponiambiabkuwa hajakiandika.

Hapohapo nikaanza kuweleza mbinu rahisi ya kuandika kitabu bila kutumia nguvu kubwa.

Nilimwuliza. Kwa siku unachati na kutuma SMS ngapi?

Nikamwambia Sasa aikiliza. Ni kweli unaposikia kitabu lazima tu uogope. Maana kitabu tu Kama kitabu utakuta kina kurasa 200 au zaidi…

Sasa ukifikiria Hilo utajikuta unakwama.

Ebu fikiria kitabu kama kuchati.  Na kila siku uandike ujumbe mfupi tu wenye maneno 100. Ambapo kwa siku ya kawaida wakati unachati kuandika maneno 100 siyo kitu kikubwa Sana. Na hata wewe ukiandika maneno 100 huoni kama issue yoyote ile.

Sasa kitabu pia kiandike hivyo..

Kiandike kama unachati vile..

Ukiandika maneno 100 kila siku kwa mwaka Ni sawa maneno 36,000/-
Sijui unanielewa?

Sasa ebu fikiria huyu msomaji wa kitabu cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO angekuwa ameazimia kuandika maneno 100 tu kila siku tangu mwaka 2020. Leo hii so agekuwa anakaribia kufikisha maneno elfy sabini?

Kitabu chenye maneno elfu sabini ni kitabu kikubwa chenye kurasa kuanzia 400 na kuendelea. Huyu jamaa angekuwa tayari anamalizia kuandika kitabu chake

Na wewe hivyo ndivyo unaweza kuandika kitabu chako.

Ukweli ni kwamba usipoanza kuandika kitabu chako, miaka miwi kutoka Sasa bado utakuwa unakwama na kusema kuwa Nina ndoto ya kuandika kitabu.

Amua leo kuwa unaenda kuandika kitabu. Hata ukiandika maneno 50 tu.  Ukifanya hivyo kila siku utajikuta mbali.

Mimi kutoka hapa mji kasoro bahari, Morogoro sina la ziada.

Naitwa
Godius Rweyongeza
Tukutane baadaye kwenye makala nyingine.

Makala ya leo imeletwa kwako kqa udhamini mkubwa wa kitabu cha JINSI YA KUWA MWANDISHI MBOBEVU NDANI YA SIKU 30 . Kupata kitabu hiki tafadhali lipia 5000 tu kwenda 0755848391 jina Ni GODIUS RWEYONGEZA. Utatumiwa ebook ndani ya dakika 5.

UKINUNUA KITABU HIKI, UNAWWZESHA MAKALA NYINGINE NZURI NA BORA ZAIDI KUENDELEA KUANDALIWA KAA AJILI YAKO.


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X