Kwanza ni kwamba, KIPAJI hakiazimwi kama nguo. Ni kitu ambacho unazaliwa nacho.
Pili, kwa kuwa kipaji tunazaliwa nacho hivyo hukilipii gharama yoyote kuwa nacho. Kitu hicho kinafanya kipaji kuwa na bei rahisi sana kuliko chumvi, pengine ndio maana watu wengine hata hawakithamini wala kukipa kipaumbele maishani mwao.
Tatu, kipaji huwezi kukitumia ukakimaliza. Kadiri unavyokitumia kipaji chako ndivyo unavyozidi kukiboresha na kukifanya kuwa bora zaidi. Ukisikia wanasema mtu fulani ameshuka viwango kwenye kutumia kipaji chake, basi ujue kuna namna anajibana kwenye kukitumia.
Kipaji ni kama misuli ya mwili, kadiri unavyokitumia, ndivyo inazidi kuimarika zaidi, usipoitumia inafhoofu.
Umekuwa nami,
GODIUS RWEYONGEZA
Hakikisha Umesubscribe kwenye Channel yangu ya youtube kwa KUBONYEZA HAPA
Jiunge na mfumo wa kupokea makala maalumu kwa njia ya barua pepe kwa KUBONYEZA HAPA
Jipatie nakala za vitabu vyangu vya kiswahili kwa KUBONYEZA HAPA
Kama ungependa kujifunza kuhusu uandishi kutoka kwangu wasiliana nami kwa 0755848391
kila la kheri
One response to “Mambo MATATU USIYOYAFAHAMU KUHUSU KIPAJI”
[…] Mambo Matatu Usiyoyafahamu Kuhusu Kipaji […]