Kwani wewe unasemaje?


Habari ya leo,

Mwezi wa tisa mwaka 2016, nilianza kuandika makala kwenye blog ya songambele na baada ya hapo niliendelea mbele zaidi na kuandika vitabu, nikaandika magazetini, nikatoa mada kwenye redio na runinga na hata kuandaa mafunzo kwenye YouTube.

Kwangu hizi zote zimekuwa ni tuzo za hatua ya kwanza niliyochukua na kuanza kuandika mwaka 2016.

Imani yangu ni kuwa lazima kwenye maandiko yangu au mafunzo yangu, utakuwa umewahi kupata kitu chochote ambacho unafanyia kazi au ambacho kimekusaidia.

Kama hilo ni kweli, basi leo ningependa kupata mrejesho wa maandishi kutoka kwako. Imani yangu kuna wengine ambao wangependa pia kusikia kitu kama hiki.

Ni kitu gani umependa? Kitu gani kimekuwa msaada kwako? Je, vitu ambavyo nilifundisha kwenye kitabu au makala vilikuwa na msaada?

Ulipenda jinsi kitabu fulani kilivyokuwa?  Ni kitu gani unadhani Kama kingeongezwa kingefanya kitabu hicho kuwa bora zaidi? Tunaomba maoni yako HAPA

Mara zote napenda mrejesho, na ninapenda kuboresha huduma na bidhaa zangu ili ziweze kuwa zenye manufaa kwako na kwa wengine zaidi.

Maoni yoyote yanakaribishwa.

Ni Mimi
Godius Rweyongeza
+255755848391
(www.songambeletz.com)
MOROGORO-TZ

BONYEZA HAPA kuweka maoni yako


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X