Kitu Kimoja Ambacho Hujawahi Kuambiwa kuhusu Kufanya Makubwa


 

Kama unataka kufanya makubwa, unapaswa kuwa tayari kuishinda hofu na uoga unaokukabili unapoanza kufanya kitu hicho mwanzoni.

Nakumbuka Kuna wakati nilikuwa naogopa na  kujiuliza kwamba nitaongea nini nikukutana na mtu fulani. Ila cha kushangaza muda kidogo baada ya kukutana na mtu huyo mazungumzo yalikuwa yanajiendesha yenyewe kiasi kwamba nilikuwa sijiulizi nitaongea nini.

Hapo ndipo nilipogundua kuwa mazungumzo yanakuwa rahisi unapoanza kuzungumza.

Wakati mwingine nilikuwa najiuliza hivi nitaanzaje kuandika? Ila nilipokuwa naanza, ndipo mambo yalikuwa yanakuwa rahisi. Kumbe, kuandika ni rahisi unapoanza kuandika.

Nilikuwa rafiki yangu aliyekuwa anapenda kufanya mazoezi. Kila nilipokuwa nikijipanga kuanza, nilikuwa najihoji, hivi itakuwaje. Mbona Kama mwili hautaki kufanya mazoezi? Baadaye nilikuja kugundua kuwa mwili wenyewe unapenda kufanya mazoezi pale unapoanza kufanya mazoezi.

Kitu hiki kinafanya kazi hata kwa vitu vingine kwenye maisha. Urahisi wa jambo haupatikani pale unapoanza bali kadiri unavyoendelea kukifanya hicho kitu. Kuna vitu ni vigumu mwanzoni, vigumu zaidi katikati ila rahisi mwishoni.

SOMA ZAIDI: KONA YA SONGA MBELE; IKO WAPI MOTISHA YA JANUARI MOSI?.🤷🏽‍♂🤷🏽‍♂

Zijue Aina Mbili Za Mbadiliko

Umekuwa nami rafiki yako wa ukweli Godius Rweyongeza

Hakikisha Umesuscribe kwenye Channel yangu ya youtube kwa KUBONYEZA HAPA

Jiunge na mfumo wa kupokea makala maalumu kwa njia ya barua pepe kwa KUBONYEZA HAPA

Jipatie nakala za vitabu vyangu vya kiswahili kwa KUBONYEZA HAPA

Kama ungependa kujifunza kuhusu uandishi kutoka kwangu wasiliana nami kwa 0755848391

kila la kheri


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X