Huyu ndiye mtu anayeweza kukusaidia kufanikisha malengo yako


 

Umewahi kujiuliza, “ni mtu gani ambaye anaweza kunisaidia mimi kufanikisha malengo yangu?” Siku ya leo ningependa nikwambie kuwa mtu pekee anayeweza kukusaidia wewe kufanikisha malengo yako ni wewe mwenyewe.

Na unaweza kufanikisha hili kwa;
1. Kwanza kujituma na kufanya kazi kwa bidii ili lengo litimie. Usiweke lengo na kusubiri tu bila ya kulifanyia kazi.

2. Kutengeneza  konekisheni unazohitaji ili lengo lako litimie.

3. Kulipa gharama inayohitajika ili kutimiza lengo lako. Ili lengo lako litimie unapaswa kuwa tayari kulipa gharama inayoendana na lengo Hilo. Kumbuka kuwa huwa hakuna mlo wa bure (there is no free lunch). Kadiri utakavyolipa gharama mapema, ndivyo utakavyoweza kufikia kengo lako mapema. Kadiri utakavyochelewa kulipa gharama ndivyo utakavyojichelewesha kufikia lengo lako pia. Na ukikwepa kulipa gharama leo, fahamu kuwa kuna siku utakazimika kuilipa hiyo gharama hata kama itakuwa uzeeni.

4. Fanya kitu kila siku hata kama ni kidogo kitakachokupeleka wewe kwenye kufanikisha lengo lako.

5. Jifunze kupitia usomaji wa vitabu mambo ambayo yanaweza kukusaidia wewe kufanikisha malengo yako. Na kisha yaweke katika vitendo.

Hivyo basi, naomba nikukumbushe kuwa jukumu la kufanikisha malengo yako ni la kwako siku zote, Wala siyo la mjomba, shangazi au serikali. Ukishinda ni juu yako. Ukishindwa pia ni juu yako.

SOMA ZAIDI: NI MARUFUKU KUKATA TAMAA

Nakushukuru Sana kwa kuweza kusoma andiko hili mpaka mwisho. Umekuwa nami rafiki yako wa ukweli Godius Rweyongeza

Hakikisha Umesubscribe kwenye Channel yangu ya youtube kwa KUBONYEZA HAPA

Jiunge na mfumo wa kupokea makala maalumu kwa njia ya barua pepe kwa KUBONYEZA HAPA

Jipatie nakala za vitabu vyangu vya kiswahili kwa KUBONYEZA HAPA

Kama ungependa kujifunza kuhusu uandishi kutoka kwangu wasiliana nami kwa 0755848391

 Kupata nakala ngumu ya kitabu cha KUTOKA SIFURI MPAKA KILELENI na kitabu cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO basi tuma ujumbe au piga kwa 0755848391

Kutengenezewa blogu yako kitalaamu tuwasiliane kwa 0755848391

kila la kheri


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X