Mambo Matano Unayopaswa Kufahamu Ili Utengeneze Marafiki Wazuri Na Wa kudumu


Marafiki ni watu wa muhimu Sana kwenye maisha yetu ya kila siku. Wanatusaudia kufanya mambo mengi Sana. Imegundulika pia kuwa marafiki wazuri ni chanzo cha furaha miongoni mwa watu. Huku marafiki wabaya wakiwa ni chanzo cha huzuni na karaha. Siyo Hilo tu marafiki wazuri wanaweza kukufanya usonge mbele na kufanikisha malengo yako au la urudi nyuma na hivyo kushindwa. Jim Rohn aliwahi kunukuluwa  akisema kuwa wewe ni matokeo ya watu watano waliokuzunguka. Hii ndio kusema kwamba kama umezungukwa na vilaza watano, basi wewe utakuwa ni kilaza wa sita. Kama umezungukwa na wawezekazi watano basi wewe utakuwa mwekezaji wa sita. Hivyo hivyo, kama umezungukwa na wachapakazi watano basi wewe unakuwa mchapakazi wa sita. Hivyo, ni muhimu sana tufahamu sanaa ya kutengeneza marafiki wazuri. Maana kipato chako, elimu, uelewa na hata maamuzi unayoyafanya yanaathiriwa sana na wale watu waliokuzunguka.

1. Kama unataka marafiki wazuri, anza wewe kuwa mzuri. Huu ni ujumbe kuntu Sana ambao unapaswa kuufahamu mara moja. Huwezi kuwa unahitaji marafiki wazuri wakati wewe mwenyewe unaendelea kufanya mambo ya hovyohovyo na yasiyoeleweka. Anza kuwa mzuri, marafiki wazuri watakuja.

2. KUWA NA MUDA WA KUJENGA MAHUSIANO
Urafiki haujengwi kwa siku moja wala Wala haujujengi wenyewe bali unajengwa. Hivyo, hakikisha unatenga muda wa kufanya hivyo.

3. KUWA MAKINI KUCHAGUA WATU AMBAO MNAENDANA KWA MAONO
Ikumbukwe kuwa miaka mitano ijayo utakuwa jinsi ulivyo, isipokuwa kwa vitu viwili tu. Watu unaokutana nao na vitabu usomavyo. Hivyo, basi chagua marafiki ambao watakusaidia wewe kuweza kufikia malengo yako wala siyo wale watakaokuangusha.

4. KUWA NA VIGEZO
Kuna vitu ambavyo unapaswa kuvijua. Yaani, kuwa ikiwa mtu atafanya kitu fulani Basi mimi n yeye  urafiki Basi.

5. KAMA HUJAPATA MARAFIKI WAZURI BASI VITABU VINAWEZA kuwa Marafiki Wazuri kwako. Hivyo basi tumia muda mwingi ukiwa unasoma vitabu. Kusoma vitabu kunakukutanisha na watu wengi hata Kama wapo mbali.

Nakushukuru Sana kwa kuweza kusoma andiko hili mpaka mwisho. Umekuwa nami rafiki yako wa ukweli Godius Rweyongeza

Hakikisha Umesubscribe kwenye Channel yangu ya youtube kwa KUBONYEZA HAPA

Jiunge na mfumo wa kupokea makala maalumu kwa njia ya barua pepe kwa KUBONYEZA HAPA

Jipatie nakala za vitabu vyangu vya kiswahili kwa KUBONYEZA HAPA

Kama ungependa kujifunza kuhusu uandishi kutoka kwangu wasiliana nami kwa 0755848391

 Kupata nakala ngumu ya kitabu cha KUTOKA SIFURI MPAKA KILELENI na kitabu cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO basi tuma ujumbe au piga kwa 0755848391

Kutengenezewa blogu yako kitalaamu tuwasiliane kwa 0755848391

kila la kheri



Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X