Deprecated: Constant FILTER_SANITIZE_STRING is deprecated in /home/songambele/public_html/wp-content/plugins/blogger-to-wordpress-redirection old/b2w-redirection.php on line 91
Edius Katamugora Afunguka Mazito Kuhusu Kitabu Cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO - SONGA MBELE

Edius Katamugora Afunguka Mazito Kuhusu Kitabu Cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO


  

 Asema Ni kitabu Bora Kuwahi Kuandikwa Kwenye Eneo Lake

Edius Katamugora ni mwandishi mbobevu akiwa ameandika vitabu kadhaa kwenye maendeleo binafsi. Amepata nafasi ya kusoma kitabu cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO na haya hapa ndiyo anayosema;

“Wakati ujao unamilikiwa na wale wanaoamini katika uzuri wa ndoto zao,” alisema Eleanor Rososevelt mke wa aliyewahi kuwa rais wa Marekani Franklin D. Roosevelt. 

Je, wewe una ndoto na unaamini kwamba inaweza kuwa kweli? Kama ni kweli basi kitabu hiki kinakuhusu sana lakini kama wewe pia unazo ndoto lakini bado hauamini kama zinaweza kutimia basi kitabu hiki ni mwanga katika njia yenye giza nene.

Ndoto sio kile unachokiota wakati umelala bali ndoto ni kitu kinachokufanya ukose usingizi. Kwa msingi huo ukiendelea kulala sio rahisi kutimiza ndoto zako, bali ukiamka unaweza kuzifanya ndoto zako kuwa kweli.

Baada ya Mama Teresa kufanikiwa na kuwa maarufu kwa sababu aliwahudumia wagonjwa na watu waliokuwa wakifa katika mitaa ya Calcutta, India, watu ambao aliwahamasisha walimtafuta. Muda mwingi walisema, “Ooh Mama Teresa! Nataka kufanya unachokifanya” Nataka kuacha kila kitu ninachomiliki na kujiunga na kazi yako!” Muda wote alikuwa akiwajibu kwa maneno haya matatu, “Tafuta Calcutta yako.”

 Kwa lugha rahisi tunaweza kusema “Fuata ndoto yako” ni huyu huyu mama Teresa aliyesema, “Kama kila mmoja akisafisha uwanja wake dunia nzima itakuwa safi” kwa mantiki hiyo kama kila mtu akifanya jambo kuhusu ndoto yake dunia inaweza kuwa sehemu nzuri sana.

Binafsi naamini kwamba kila mtu anazo ndoto ambazo anatakiwa kuzifanyia kazi, mwandishi wa kitabu hiki ameandika kwa uzuri na ubora wa juu mbinu na namna mbali mbali za kuzifikia ndoto zako.

Wenye ndoto ni wale watu wanaosema maneno, “Liwalo na liwe” lazima nitimize ndoto zangu. Nilipokuwa natizama filamu ya kizungu iitwayo The Shawshank Redemption nilijifunza kitu kimoja kwamba ukiamua kufanya chochote unaweza kukifanya kikubwa ni kuweka nia na matumaini. Andy Dufresne ambaye aliweza kutoroka gerezani anasema, “Kuwa Bize Ukiishi au kuwa bize ukifa ” maneno haya yamewekwa wazi na mwandishi anapotukumbusha kwamba kuna kitu tunahitaji kufanya kwa ajili ya ndoto zetu, lazima siku tukiondoka tuniani tuache alama.

Mwandishi wa kitabu hiki amenitafakarisha sana aliposema, huwa tukifa wanasema, Äpumzike kwa amani,” anaendelea kusema kwamba “Kuna watu hawasitaili kuambiwa ampumzike kwa amani maana muda wao mwingi hapa duniani ulikuwa wa kupumzika”.

Amka sasa usibweteke anza kuzifanyia kazi ndoto zako. Kumbuka kwamba watu wote waliofikia ndoto kubwa hawakuanzia pakubwa walianzia padogo. Kuna aliyewahi kusema, “Kinachoanzia juu ni kaburi tu”, hata kama vitu fulani havijakamilika wewe anza tu.

Kwenye safari ya kuifikia ndoto yako au kuzifikia ndoto zako lazima ukumbane na vigingi, lakini kumbuka hakuna ushindi bila mapambano lazima uyashiriki mapambano hayo.

 Kila hatua mpya inahitaji wewe mpya na mbinu mpya lazima uwe umejipanga.

Inawezekana umekua ukisaidia kutimiza ndoto za wengine, sasa ni wakati wako kuamka na kuanza kufanyia kazi ndoto zako, unaanzaje kuzifanyia kazi ndoto hizo, mwongozo ulio katika kitabu hiki ni dira tosha iliyosheheni madini na ramani ya kukupeleka kule unakotaka kufika na hata zaidi.

Nafikiri kitabu hiki ni kitabu bora zaidi kukisoma katika vitabu vya Kiswahili nilivyowahi kusoma kuhusu nama ya kuzifikia ndoto zangu, kimenijenga sana na nimepata vitu vingi vipya ambavyo kweli sikuvifahamu.

Mwandishi wa kitabu hiki, Godius Rweyongeza ni mtu ambaye nimemfahamu na kumfuatilia kwa muda mrefu, mambo mengi anayoyaandika ni yale ambayo tayari anayafanyia kazi na yameleta matokeo hivyo ukifuata kile alichoandika ndugu Godius hautaacha kufika mbali sana.

Nikusihi ukisome kitabu hiki si mara moja bali mara nyingi uwezavyo kwani madini yaliyo humu ni lulu tosha ya kukuvusha wewe katika hatua uliyopo na ukafika katika hatua zingine.

Pia maneno unayoyasoma humu yaweke katika matendo, kuwa na vitu vingi kichwani bila kuviweka katika matendo ni sawa na kuwasha gari bila kuliondoa, haufiki kokote. Ukitaka kufika mbali fanya kwa matendo.

Mwisho wa yote kumbuka, dunia inawapokea kwa mikono miwili wale wanaofanya mambo katika matendo na kwa ubora wa hali ya juu, kwa msingi huo naunga hoja ya Ralph Waldo Emerson aliyewahi kusema, “Kama mtu akiandika kitabu kizuri, akahubiri mahubiri mazuri, au akatengeneza mtego wa panya mzuri kuliko jirani yake, hata akijenga nyumba yake msituni, dunia nzima itatengeneza njia hadi mlangoni kwake.”

Utumie muda wako vizuri maana kila kitu ni zao la muda. Vitu vyote vizuri unavyoviona vilitengenezwa ndani ya muda fulani. Tumia muda wako kujiendeleza na kujifunza kuhusu mambo yanayohusu ndoto zako, tumia muda wako kwa wengine na mwisho tumia muda wako kutengeneza huduma au bidhaa fulani. Hivi ndivyo watu wote wenye ndoto kubwa walivyofanya na kufikia hatua za juu.

Nampongeza sana na tena sana ndugu Godius Rweyongeza kwa kitabu hiki kizuri kinachoelimisha, hamasisha, tafakarisha lakini pia kinaburudisha kupitia stori mbalimbali alizotuwekea humu.

 *Ukianza kusoma kitabu hiki hutokichoka!* 

Ndimi,

Edius Katamugora (Kijana wa Maarifa)

Mwandishi kitabu cha Yusufu Nina Ndoto. 

Rafiki yangu, bila shaka umeona aliyosema Edius Katamugora. Binafsi sima Cha kuongeza labda kukwambia tu kuwa sasa ni zamu yako kupata kitabu hiki. Nakala ngumu ya kitabu hiki ni elfu 20 tu. 

Ukiihitaji soft copy ya kitabu hiki pia inapatikana pamoja na vitabu vingine Viwili kwa elfu 19,999.

Karibu Sana. Tuwasiliane kwa 0755848391 karibu


2 responses to “Edius Katamugora Afunguka Mazito Kuhusu Kitabu Cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO”

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X