Rafiki yangu, hongera sana kwa siku hii ya kipekee sana.
Ni siku sasa zimepita tangu uzinduzi wa kitabu cha KUTOKA SIFURI MPAKA KILELENI.
Nakumbuka ilikuwa ni tarehe 25 mwezi wa 9 2017, mtu wa kwanza aliposoma hicho kitabu.
mmoja wa watu waliosoma hicho kitabu alikuwa ni Octavian, yeye alikuwa na haya ya kusema siku chache baada ya kuanza kukisoma
Nimesoma kitabu cha kutoka sifuri mpaka kileleni. Cha ajabu nikiwa bado ukurasa wa utangulizi, nimesoma sentensi, nikaona malengo niliyoyaweka ndani ya miaka miaka minane yanaenda kukedamilika ndani ya miaka minne. Sasa sijui nikija kufika ukurasa wa mwisho itakuwaje. Big up sana ndugu yangu Godius
Kitu kikubwa nikichonacho kwako siku ya leo ni juu mabadiliko yabjalada la kitabu. Kama unavyofahamu jalada la awali lilikuwa hili hapa.
Hata hivyo sasa hivi jalada letu ndio hili hapa
Kwa hiyo hili jalada ambalo leo ndio kwanza unaliona, ndio linaenda kuonekana kwenye kitabu.
Mabadiliko ya jalada ni ishara ya mabadiliko makubwa ndani ya kitabu. Ninaenda kusa nakujulisha zaidi juu ya mabadiliko haya siku zijazo.
kwa leo nilitaka nikujuze haya mabadiliko ya jalada. Hata hivyo unapaswa kufahamu kwamba, mabadiliko ya jalada ni ishara ya mabadiliko ya kilicho ndani ya kitabu.
kwa maelezo zaidi soma zaidi: KITABU; KUTOKA SIFURI MPAKA KILELENI
Ni mimi anayejali mafanikio yako,
Godius Rweyo geza
0755848391
2 responses to “YAH: MABADILIKO YA JALADA LA KUTOKA SIFURI MPAKA KILELENI”
It is a very interesting blog, so keep it up.
karibu sana. Endelea kuitembelea kila siku. Makala mpa zinawekwa hapa kila siku