Kitu Kimoja Kitakachotokea Endapo Utakuwa Mlalamikaji


Rafiki yangu hongera sana kwa siku hii ya leo na ya kipekee sana. Kama umekuwa mtu wa kulalamika leo kuna vitu viwili ambavyo huwa vinatokea pale mtu anapolalamika.
Kwanza kabisa unapolalamika unakuwa unawaonesha watu wengine fursa ambazo wewe mwenyewe umeshindwa kuzitatua. Hivyo watu wengine wanaweza kutatua kurekebisha hicho kitu ambacho wewe mwenyewe unalalamikia. Ni wazi kwamba matatizo na changamoto ambazo mtu unakuwa unalalamikia ni fursa za watu wengine.
Hata ukiiangalia historia yote. Ugunduzi wote ambao umefanyika, umefanyika ili kutatua matatizo ambayo yalikuwepo hapo awali.
Biashara zote ambazo zimeanzishwa,  zimeanzishwa ili kutatua changamoto ambazo zilikuwpo hapo awali.
Wajasiliamali wote na wafanyabiashara wote unaowafahamu, kazi iyao ni moja tu. kutatua matatizo.
Kwa hiyo wewe unapolalamika ni wazi kwamba watu wa aina hii wataichukua hiyo changamoto na kuangalia namna ambavyo wanaweza kuitatua na ili waisaidie jamii. Ikumbukwe kwamba ujasiliamali ni kutatua matatizo ya watu.
Kuanzia leo hii kitu chochote kile ambacho unaona unataka kulalamikia, nenda hatua ya ziada ili uweze kukibadili. kama huwezi kukibadili achana nacho.

SOMA ZAIDI: Kama Tatizo Ni Nyota; Ya Kwako Imeenda Wapi?

Ni mimi anayejali mafanikio yako
GODIUS RWEYONGEZA

KUWA MIONGONI MWA WATU AMBAO WANAPOKEA MAKALA MAALUMU KWA WATU MAALUMU KWA KUBONYEZA HAPA

SUBSCRIBE KWENYE CHANNEL YANGU YA YOUTUBE HAPA


JIUNGE NAMI KWENYE NURU ANGAZA

,

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X