Kiu Muhimu Unachopaswa Kujifunza Na Kuvifahamu Kiundani


Hongera sana rafiki yangu kwa siku hii njema sana. Leo imekuwa siku bora sana kwetu, ni siku ya kipekee sana ambayo unapaswa kuitumia kufanya kitu ambacho kitabadili maisha yako na kukufanya usonge mbele.

Kuna kitu kimoja tu ambacho unapaswa kukifahamu haswa na unapaswa kukifahamu kiundani. Na kitu hiki ni MAUZO.
Kila mtu katika maisha huuza. Iwe ni mtoto au mtu mzima. Iwe ni amesmomea kuuza au hajasomea. Ila kila mtu anauza.

Iko hivi unapoongea na mtu ukijaribu kumshawishi akubari kile unachomwambia ujue unauza mawazo yako.
Kama wewe ni mwanasiasa unashawishi watu wakupigie kura ujue kwamba upo unauza Sera.
Kama wewe ni mrumishi unahubiri neno la Mungu, ujue upo unauza.
Hata kama unamshauri mtu afanye mabaya bado wewe unauza
Kama wewe ni Mwalimu unafundisha   wanafunzi waelewe na wafaulu mitihani, jua kwamba unauza.
Kama wewe huna kazi unatembea na vyeti kutafuta kazi jua kwamba upo unauza kisomo chako ili ukubariwe na kupewa kazi.
Kama wewe ni unatafuta mchumba na ungependa akukubalie basi jua kuna kitu unauza.

Naamini, mpaka hapo ushaelewa ni kuuza ni nini!
Kwa hiyo kuanzia leo jifunze, jifunze jifunze kuuza.

Kwa siku Chache zijazo, tutaendelea kujifunza juu ya suala zima la kuuza na kwa jinsi gani litakusaidia kufikia makubwa.

Umekuwa nami,
Godius Rweyongeza
0755848391
KUPATA KITABU CHA KUTOKA SIFURI MPAKA KILELENI BONYEZA HAPA

HUDUMA NYINGINE UNAZOWEZA KUPATA KWANGU HIZI HAPA
KUPATA MAKALA MAALUM KWA WATU MAALUM KILA WIKI BONYEZA HAPA


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X