Kitu Muhimu Unachopaswa Kurekebisha Kwenye Biashara Yako


Ni siku nyingine bora sana rafiki yangu. Hongera sana kwa siku hii ya leo.

Katika biashara kuna mambo mengi sana ambayo unaweza kufanya. Kutunza kumbukumbu, kutafuta wateja wapya, kuuza, kutafuta watu wa kuajiri na mengine mengi. Leo hii napenda nikwambie kitu kimoja muhimu sana ambacho unapaswa kukijua kuhusu biashara yako. Na kitu hiki sio kingine bali ni ukweli kwamba biashara yako inahitaji ukaribu wako.
Kama biashara yako inaanza itahitaji uilee na kuikuza kama mtoto.
Kama tayari imekua biashara yako itahitaji kupanuka zaidi, kuongeza mauzo na kusimamiwa kwa umakini zaidi.

Kama unavyoona katika kila hatua ya ukuaji wa biashara yako, uangalizi ni jambo la muhimu sana. Jitahidi sana kuhakikisha unakuwa karibu na biashara yako muda wote. Ijue nje ndani bila kuacha kitu.
Hili ndilo jambo muhimu unalopaswa kulifahamu kuhusu biashara yako.

Asante sana rafiki yangu. Tukutane kwenye jukwaa la wanamafanikio

Umekuwa nami,
Godius Rweyongeza
0755848391
KUPATA KITABU CHA KUTOKA SIFURI MPAKA KILELENI BONYEZA HAPA

HUDUMA NYINGINE UNAZOWEZA KUPATA KWANGU HIZI HAPA
KUPATA MAKALA MAALUM KWA WATU MAALUM KILA WIKI BONYEZA HAPA


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X