Hii Ndio Kauli Ya Kishujaa Unayoweza Kujiambia Kila Kukicha


Kwa siku mwanaume anasemekana kuongea maneno yasiyopungua 7,000 huku mwanamke akiongea maneno zaidi ya elfu 21. Wakati kauli na maneno  yaliyo mengi yanayoongelewa mara nyingi huwa ni stori za kawaida, unapaswa sasa kubadilisha na kuanza kuongea kauli za kishujaa. Na leo hii nakuletea kauli moja muhimu sana ambayo ni ya kishujaa ambayo unapaswa kuitamka kila siku. Kauli yenyewe ni hii hapa,

“Nitakuwa king’ang’anizi mpaka nishinde. Nimekuja duniani kushinda wala kushindwa sio sehemu ya maisha yangu.  Mimi sio kondoo ambaye nasubiri kuongozwa na mchungaji. Mimi ni simba, nakataa kata kata kutembea, kuongea na kuishi na kondoo.  Nitakuwa king’ang’anizi mpaka nishinde”.

Ebu iandeke kauli hii sehemu. Isome na kuirudia kila iitwayo asubuhi, mchana mpaka jioni.

Nakutakia wakati mwema sana

Soma Zaidi:  Hii Ni Kauli Unayopaswa Kuiepuka Maishani Mwako

Ndimi,
Godius Rweyongeza
0755848391

KUPATA KITABU CHA KUTOKA SIFURI MPAKA KILELENI BONYEZA HAPA


HUDUMA NYINGINE UNAZOWEZA KUPATA KWANGU HIZI HAPA
KUPATA MAKALA MAALUM KWA WATU MAALUM KILA WIKI BONYEZA HAPA


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X