Deprecated: Constant FILTER_SANITIZE_STRING is deprecated in /home/songambele/public_html/wp-content/plugins/blogger-to-wordpress-redirection old/b2w-redirection.php on line 91
Ukweli Kuhusu Safari ya Mafanikio - SONGA MBELE

Ukweli Kuhusu Safari ya Mafanikio


Safari ya ya mafanikio sio ya mchezo mchezo, bali safari ambayo hukuitaji uwe makini na ujiandae sawasawa na kujitoa. Kama utaanza safari ya kimafanikio bila kujitoa sawasawa, na kujiandaa pale utakapokutana na vikwazo mbalimbali kama vile kukata tamaa, kukatishwa tamaa, kupingwa, na visingizio utakwama. unahitaji uwe umejipanga kisawasawa.

Unahitaji kuwa umeweka malengo na mipango ya jinsi gani utaanza mpaka kufikia kileleni
Unaambiwa kati ya biashara kumi ambazo huanza kila mwaka, tisa hufa ndani ya mwaka mmoja, na kati ya zile zinazoendelea moja kati ya tano ndio husimama na kuwa biashara bora ndani ya miaka mitano!!

Sasa kwa nini nasema ujipange sawasawa?
Nasisitiza kwamba ujipange sawasawa ili usije kujitoa kwenye msafara wa wana mafankio. Wengi sana hupenda kuingia katika msafara huu. Lakini wachache sana huweza kuendelea na safari. Ndio maana wahenga wakasema  “ kwenye msafara wa mamba na kenge wamo “. Sasa kenge ndo akina nani?
Kenge ni wale ambao wako tayari kujitoa mda wowote kwenye msafara wa safari.


Nifanyeje ili niweze kujipanga sawasawa?
Weka malengo. Unahitaji kuwa na malengo makubwa ambayo yatakupa msukumo katika kufanya kazi yako na kufikia mafanikio.

Ntafaidikaje kwa kujipanga sawasawa? 
Kujipanga sawasawa kutasaidia

  • Kukamilisha malengo ambayo  umekwisha jiwekea.
  • Kutokata tamaa wakati
  • Kukabiliana na kila aina ya changamoto
Sasa nifanyeje ili niweze kufikia mafanikio?
Tumeona kuwa safari ya mafanikio sio ya mchezo mchezo. Tunahitaji kuzingatia baadhi ya mambo ili yusije rukaishia njiani.
Nidhamu.
Imekuwa kawaida ya watu wengi sana kuwa wanajishughulisha na mambo mengi sana,  lakini ukosefu wa nidhamu umekuwa unasababisha watu kuwa kutofikia mafanikio.
Jenga nidhamu yako katika  kutunza muda, na matumizi mazuri ya pesa.
Jijengee utaratibu wa kusoma .
Watu wengi sana wamekuwa hawana utaratibu wa kusoma na kuongeza maarifa kila siku. Hii haina maana kwamba urudi shuleni. Bali inakuhitaji uongeze maarifa ya kukusaidia kujua mambo kadha wa kadha yanayotokea duniani, mabadiliko ya biashara zako na jinsi ya kukabiliana na mabadiliko hayo.
Ni mimi rafiki na ndugu yako
Godius Rweyonheza
Tuwasiliane 
godiusrweyongeza1@gmail.com
0755848391
Asante
Endelea kusoma makala za kuelimisha na kuhamasisha kutoka kwenye blogu hii


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X